Kagera Maji ya Shingo kwa Simba

KLABU ya Kagera Sugar imejiandaa vizuri kuelekea kwenye mchezo wao wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara utakaochezwa kesho Agosti 20 dhidi ya Simba katika uwanja wa Mkapa Dar.

Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika jana Ijumaa Makao Makuu ya TFF, yaliyopo Ilala Dar, kocha mkuu, Francis Baraza wao wamejipanga vizuri kuwakabili Simba ingawa haitakuwa rahisi kupata matokeo mazuri.

“Kwa sasa tumejipanga vizuri kwa ajili ya mechi ya kesho dhidi ya Simba na tunatarajia matokeo mazuri.

“Japokuwa Simba ni timu kubwa na imechukua ubingwa zaidi ya mara moja, sisi tumejipanga vizuri na hata ukiangalia mchezo uliopita dhidi ya Azam FC, utaona jinsi tulivyojipanga na tutafika mbali.” Alisema.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.