Zamalek Yatwaa Ubingwa wa Misri.

Klabu ya Zamalek ya nchini Misri imrfanikiwa kubeba ubingwa wa ligi kuu nchini humo maarufu kama Egypt Premier League.

Zamalek wanafanikiwa kubeba ubingwa wa ligi kuu nchini humo ikiwa ni mara ya pili mfululizo baada ya kubeba ubingwa huo mwaka 2021 hivo inakua mara ya pili mfululizo kwa kutwaa ubingwa huo mwaka huu 2022.

Zamalek wanabeba ubingwa wa Misri huku wakiwa wamebakiza michezo miwili mkononi na wanatawazwa mabingwa kwasababu hata wakipoteza michezo miwili iliobaki hawafikiwi kwa alama na anayeshika nafasi ya pili ambae ni klabu ya Pyramids yenye alama 68 huku klabu ya Zamalek ikiwa na jumla ya alama 76.

klabu ya Zamalek inabeba ubingwa huku mahasimu wao wakubwa klabu ya Al Ahly wakiwa wanachechemea huku wakiwa wanashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi hiyo. Zamalek sasa wanakua na jumla ya mataji 14 ya ligi kuu nchini humo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.