Mshauri Mkuu wa masuala ya Uongozi ya klabu ya Yanga, Senzo Mbatta amesifia viwango vya wachezaji wa Simba walivyoonyesha kwenye mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika.
“Nawaheshimu wachezaji wote niliofanya nao kazi, ukiwaangalia kupitia mechi za CAF, Manula, Kapombe, Chama, Luis (Miquissone), Edward Manyama wa Namungo na Wawa (Paschal) wamefanya vizuri na wanahitaji hatua kubwa zaidi.
Kauli hiyo aliiandika kupitia ukurasa wake Instagram na imeungwa mkono na wachangiaji wengi katika ukurasa wake baada ya kuonyesha kukubali kile kilichofanywa na wachezaji wa timu pinzani.
Ikumbukwe Senzo kabla ya kujiunga na Yanga alikuwa Mtendaji Mkuu wa Simba (CEO) na alifanya kazi na wachezaji hao.
Bonasi ya 50% Kila Siku Katika Kasino za Evoplay hapa Meridianbet.
Meridianbet na Evoplay Kasino wanakupa bonasi ya 50% ya kiasi utakachoweka katika akaunti yako leo. Unasubiri nini ni wakati wa kupiga pesa sasa na Mabingwa.
Nice
Vizuri