Klabu ya Simba SC leo imemtangaza mshambuliaji wao mpya wa kimataifa kutoka nchini Serbia Dejan Georgijević ambaye amesaini kandarasi ya miaka miwili kuitumikia klabu hiyo.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa mwenye miaka 28 kutokea serbia, alikuwa anaichezea klabu ya NK Domzale mbayo inashiriki ligi kuu ya nchini slovenia, kabla ya kusajiriwa na klabu ya Simba.
Dejan Georgijević ameichezea NK Domzale michezo 17 na kufanikiwa kufunga magoli 4 kwenye mashindano yote ndani ya msimu wa 2021/22. Mpaka sasa amevichezea vilabu mbalimbali barani Ulaya, lakini hii ndio mara yake ya kwanza kucheza kwenye ardhi ya Afrika.
Dejan ni chaguo la kocha wa Simba, ambaye aliyomba klabu hiyo kuweza kufanikisha usajiri wa mshambuliaji huyo, ili kuongeza nguvu kwenye kikosi hicho ambacho kimewafungulia milango ya kutokea baadhi ya washambuliaji wake akiwemo Mugalu na kagere kwenye dirisha hili la usajiri.
MWAKA | TIMU | MICHEZO | MAGOLI |
---|---|---|---|
2010–2011 | Zemun | 6 | 0 |
2012–2014 | Teleoptik | 58 | 8 |
2014–2015 | Spartak Subotica | 16 | 3 |
2015–2016 | Inđija | 27 | 14 |
2016–2018 | Voždovac | 41 | 12 |
2018–2021 | Ferencváros | 7 | 1 |
2019 | Partizan (mkopo) | 3 | 0 |
2019 | Irtysh Pavlodar (mkopo) | 16 | 2 |
2021 | Velež Mostar | 19 | 5 |
2021–2022 | Domžale | 17 | 4 |