Gabriel Jesus ameitaka Brazil kudhihirisha kwa mara ya nyingine kama wanaweza kushinda bila uwepo wa Neymar baada ya kuthibitika nyota huyo ataukosa mchezo wa kufuzu kucheza World Cup 2022 dhidi ya Venezuela.
Mchezaji huyo wa Selecao anayevalia jezi namba 10 mgongoni anapambana na majeraha yaliyopelekea akose michezo mitatu ya Paris Saint- Germain katika mashindano yote, ukijumuishwa mchezo waliyopteza katika Champions League dhidi ya RB Leipzig.
Neymar mwenye umri wa miaka 28 kwenye nusu fainali ya kombe la dunia mwaka 2014 alikosa mchezo dhidi ya Ujerumani na dunia ikishuhudia Brazil ikipokea kipigo cha aibu wakiwa nyumbani.
Lakini vijana wa Tite pia hawakuwa na Neymar mwaka uliyopita kwenye fainali ya Copa America na Brazil ilishinda kombe hilo na Jesus haamini kama timu yake itakua na la kujitetea kama wasipo shinda.
“Kimsingi tunaongelea umuhimu wa Neymar akiwa katika timu ya taifa na klabu, kile anachotoa kila siku, Mimi ni shabiki yake mkubwa alisema fowadi huyo wa Manchester City.
“Tukiwa na Neyamr tunakaribia zaidi ushindi lakini the Selecao wanaweza kucheza na kushinda bila Neymar.
“Mara nyingi tumekuwa tukitaka uwepo wake uwanjani kwa sababu anafunga na kutoa asisti, lakini asipokuwepo inatubidi tugawane majukumu.
Jesus ambaye alifunga magoli yote na baadaye kutolewa nje katika fainali ya Copa America anajiandaa kutumia nafasi yake baada ya kukosa michezo iliyopita wakati wa mapumziko ya mechi za kimataifa.
“Mara zote nataka kucheza na kuisadia timu na wakati huu nimekuja nikiwa sawa 100% nipo tayari kuisadia timu yangu.
Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!



magdalena
kabisa maana wapo wachezaji wazuri na bora kuliko neymar
Adelta
Good news
Nasra
Gud news
Khadija
Asante kwa makala
Dorophina
Inaweza ikawa neymar ndio ameibeba timu ndiomaana awawezi bila neymar
Tatu
Brazil wanamasteka wengi ila neymar ndio kaibeba timu
Carolyn
Safi Sana.Jesus.msiishi kwa kumtegemea fulani .mtafeli
Mwajumah
Safi sana hakuna kuishi kwa kumtegemea mtu
Angelina
Ni jambo zuri kujiamin bila uwepo wa Nymar
Samira
Ni vizuri kutambua hilo coz ushirikiano unatakiwa kwa wote sio kwa mtu mmoja
Elika
Ni jambo jema
Lydia Emmanuel Magoti
Nikweli kabisa Kuna wachezaji makini Sana
Fatina mfingi
Ni kweli kikosi kizima akiwezi mtengemea mtu mmoja ila akiondoka yy kunapeng tu litakiwep kwa mud tu then Mambo yatakuwa saw
Fatuma kasomo
Gud news
Saupha mohamed
Neymar ndo kiboko yao
Sabrina
Neymar jeshi
felister
habari njema
Janeflora malisa
Asnt kwa taarif meridianbet
Ester jackson
Kwenye ukweli tuseme nerymaa anamchango wake kwenye timu take yataifa ingawa inabidi kwenye timu zetu za taifa wachezaji wajifuze kucheza vema kuliko kumtegemea mchezaji wa aina yoyote ile
Rahma
Asnte kwa makala
zeiyana
ni kweli jesus yupo sahihi kila mda na wakati wake neymar hatabaki kua kama neymar lakini wasiyanye hakawa kama tegemenzi kwenye timu kila mchezaji hashike nafasi yake
Povel
Nice update
Issa
Brazil ina vipaji vingib sana na neymar amekua kama ndio character kubwa ndan ya timu