C.E.O Simba Aionya Yanga Ngao ya Jamii

Simba juzi Jumatatu kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa walitangaza rasmi majembe yao mapya na benchi lote la ufundi kuelekea msimu ujao wa 2022/23 huku pia wakitoa burudani kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya ST. George ya Ethiopia.

Jumamosi hii Simba wanatarajiwa kuvaana na Yanga katika mchezo wa ufunguzi wa ligi maarufu mchezo wa Ngao ya Jamii, unaotarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Barbara alisema: “Kwa niaba ya uongozi tunashukuru kwa sapoti kubwa ambayo mashabiki wetu wamekuwa wakituonyesha siku zote, lakini hasa katika tamasha letu la Simba Day.

“Najivunia ubora ulioonyeshwa na kikosi chetu, nadhani kila mmoja ameona ubora mkubwa wa watu tuliowasajili, hii ina maana kuwa tumejipanga kufanya makubwa msimu ujao, kwa sasa tumesahau kuhusiana na kile kilichotokea Jumatatu na nguvu yetu kubwa ni kuhakikisha tunashinda mchezo wa Jumamosi dhidi ya Yanga.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.