Neymar alisema kwamba kombe la dunia 2022 inaweza kuwa ndiyo mwisho wake kuichezea timu ya taifa ya Brazil sasa mara baada ya kutoa kauli hiyo mchezaji wa zamani wa Paris Saint-Germain Jerome Rothem amekosoa kauli yake hiyo.

Pia tunaweza kusema kwamba kauli hiyo haijaja katika wakati sahihi baada ya kukosolewa na mashabiki kufuatia kiwango chake kushuka ndani ya klabu ya PSG.
“Ujumbe wake wa hivi karibuni ni wa kutisha kwa PSG,” alisema Rothen.
“Amekosa kujitolea kwenye klabu anafanya siyo sawa”.
“Neymar ni mchezaji mzuri sana akiwa katika ubora wake lakini tatizo ni kwamba anakosa ujasiri.
“Upendo aliyonao kwa Brazil ni dhahiri,” Rothen aliendelea “anataka kushinda kombe la Dunia.
“Nafasi yake ya mwisho itakuwa ichini Qatar mwaka ujao, lakini nadhani anapaswa kukabiliana na majukumu yake.
Neymar mwenye umri wa miaka 29 aliiambia DAZN kwamba “Nadhani mwaka 2022 nchini Qatar utakuwa kombe langu la mwisho kwasababu sijui kama nitakuwa sawa kiakili na kimwili kukabiliana na soka tena.
Fanya wiki yako iwe ya kuvutia zaidi, tunaelekea Los Angeles kutengeneza mkwanja na kasino maridhawa ya LA Rouge kutoka katika kasino za mtandaoni za meridianbettz, Fursa ya kufurahi huku unajaza pochi yako.

CHEZA HAPA

