Staa Geita Gold aahidi jambo

STRAIKA wa Geita Gold, George Mpole ameahidi kupindua matokeo kuelekea kwenye mchezo wao wa marudiano wa kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Hilal Al Sahil ya nchini Sudan.

Geita Gold kwenye mchezo wa kwanza uliochezwa nchini Sudan walipoteza kwa bao 1-0 hivyo wanapaswa kushinda mabao 2-0 ili waweze kuvuka hatua inayofuata.

Mchezo huo wa marudiano unatarajiwa kupigwa kesho kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Jijini Dar.

Akizungumzia maandalizi yao, Mpole amesema kuwa “Sisi kama wachezaji tumejipanga vizuri kuelekea kwenye mchezo wetu wa kesho jumamosi.

“Tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kwa ajili ya kuja kutusapoti na sisi tunawaahidi kwamba tunaenda kupindua matokeo na kuvuka katika hatua hiyo.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.