Mbappe: Nilijiunga na PSG Ili Niweke Historia ya Champions League.

Kylian Mbappe amesema kwamba alijiunga na PSG ili aweke historia kwa kushinda taji la Champions League katika mchezo wa kukamilisha msimu dhidi ya Bayern Munich.

PSG iliyowatoa RB Leipzig katika hatua ya nusu fainali na kufanikiwa kufika fainali yao ya kwanza katika Champions League itakutana uso kwa uso na mabingwa wa Bundesliga mjini Lisbon siku ya Jumapili.

Mbappe alishawahi kufika hatua ya nusu fainali akiwa na timu ya Monaco mwaka 2017 kabla hajafanya uhamisho wa pesa nyingi na kutua PSG.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 ameonekana kuwa vizuri baada ya kupona jeraha lake la kifundo cha mguu na ameamua kuhakikisha PSG inashinda mashindano hayo makubwa ya Ulaya kwa mara ya kwanza wikendi hii.

“Sisi ni ‘underdogs’ kulingana na kila mtu anavyotuchukulia na tunapenda tukisikia hivyo. Nilicheza kwenye Fainali ya Kombe la Dunia na nilishinda. Sasa hili ni taji lingine kubwa ambalo ninataka kushinda kwenye maisha yangu. Nitapambana kama ni siku ya mwisho ya maisha yangu.

“Naamini tuna ubora sawa na Bayern Munich. Endapo Ikicheza mchezo wa kutumia nguvu, sisi pia tutakuwa na nguvu sana kuona ikiwa watapenda ladha ya dawa yao wenyewe.”

“Tuna Kocha Mjerumani ambaye anajua mbinu za Kijerumani. Anajua jinsi ya kuwashughulikia Bayern Munich.”

“Hii ndiyo sababu kwanini nipo hapa,” Mbappe aliongea na waandishi siku ya Jumamosi. “Mara nyingi nimekuwa nikitaka kuandika historia katika mpira wa Ufaransa, sasa nina fursa ya kufanya hivyo.


Drops and Wins!

Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.

Soma zaidi ucheze

43 Komentara

    Asante kwataharifa

    Jibu

    Litakua jambo zuri sana km leo utafunga na kuchukua ubingwa.

    Jibu

    Ndoto yake Leo usiku yaweza kutimia

    Jibu

    Mbappe atafanikisha tu hitajio lake la kuchukua ubingwa wa champions league asiwe na papala anatakiwa ajitume

    Jibu

    Hizo ndoto zake mbappe lakini sio kwa timu wanayo kuna nayo..!kwa Bayern munch sio kilaisi laisi hivyo yani mjipange sana

    Jibu

    Mbappe tunakuombea ukamilishe ndoto yako leo kila la kheri brooo

    Jibu

    Vizuri mbappe adi yako itatimia mpambanaji

    Jibu

    Binafsi nafurahi kuona kila mchezaji anajitoa Asilimia zote kuweza kutimiza ndoto yake, Leo utakuwa usiku mzito sana Barani Ulaya.

    Jibu

    yuko vzr sana

    Jibu

    Tunasubiri kuona maneno yake yanatafsiriwa kwa vitendo Ushindi hautakuwa rahisi kwa yeyote#meridianbettz

    Jibu

    Na Leo itabidi aikamilishe historia

    Jibu

    Ajitahidi atatimiza alichokusidia

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Sasa ni wakat kuvunja record bahat haiji mala 2

    Jibu

    Aongeze juhudi atatimiza malengo yake

    Jibu

    Mbappe Yuko vizuri na anajiamini ktk majukumu yake @meridianbettz

    Jibu

    Anajipa imani tu bayern ni moto na champion league wanalisaka patachimbika leo

    Jibu

    Leo onyesha umahiri wako

    Jibu

    Na leo usiku itabidi akamilishe historia#Meridianbettz

    Jibu

    timiza ndoto yako basi

    Jibu

    Leo mbappe ndio siku ya kuwaonesha Wana psg Mambo makubwa

    Jibu

    Mbappe kujiunga na PSG ni jambo LA msingi tena hukovatakuza kipaji

    Jibu

    Good new

    Jibu

    Timiza ndoto zako

    Jibu

    Ngoj tuone Kama dreamx can true leo kwa mbappe

    Jibu

    Kiukweli mbappe ni mchezaji mzuri sana

    Jibu

    Kila mchezaji hua anandoto katika career yake nadhani mbape ndoto yake ilikua hii.

    Jibu

    Ndoto zake zitatimia siku hadi siku

    Jibu

    Mbappe yupo viziri

    Jibu

    Talent and famous player kila la kheri ktk ndoto zake.

    Jibu

    Ndo basi tena mmesha pigwa#Meridianbettz

    Jibu

    Maoni:safiii sana

    Jibu

    mbappe ndoto zake hazikufanikiwa kutimia baada ya kupokea kichapo zidi ya bayern

    Jibu

    Vizuri

    Jibu

    Itabid aendelee kuwa na ndoto hizo maana bado kijana huyo

    Jibu

    Kujiamini ndio mpango mzima!!!

    Jibu

    Mbappe alishawahi kufika hatua ya nusu fainali akiwa na timu ya Monaco mwaka 2017 kabla hajafanya uhamisho wa pesa nyingi na kutua PSG.

    Jibu

    Mbape Yuko vzr Sana

    Jibu

    Yuko vizuri

    Jibu

    Usijar kijana kaza buti utatimiza ndoto yako

    Jibu

    Yuko vzr

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.