Si unakumbuka Giovanni Van Broickhoist alivyoisimamisha Afrika Kusini ile 2010. Wahuni wa Soweto wakakubali kuzima misokoto, wakasimama kutazama matusi yasiyokera ya ‘m-dutch’. Lile bao, hadi madaktari walisahau kuwasikiliza wagonjwa wao.

Vipi kuhusu Arjen Robben mbele ya wahispaniola 2014 pale Brazil? Namna alivomzunguka Sergio Ramos, kisha kumzalilisha Iker Cassilas, lile ni kosa la jinai. Mabao kama yale yanaweza kukunyanyua kwenye ‘kibanda umiza’, Ukarudi kulipa mara ya pili.
Tuachane na hayo. Unamkumbuka ‘superman’ Roben Van Persie? Ile siku Hispania wanakufa 5-1 pale ‘Arena Fonte Nova’. Ilikuwa mara ya kwanza Hispania wanafungwa zaidi ya mabao manne katika mchezo wa kimashindano tangu 1963. Van Persie alifunga bao la kwanza.
Hispania walikitawala kipindi cha kwanza. Penalty ya Xabi Alonso iliwaweka mbele dakika ya 27. Dakika mbili tu kabla ya mechi kwenda mapumziko, David Silva alishindwa kuitendea haki pasi ya Andres Iniesta, akaamua kuubetua mpira badala ya kutulia azisake nyavu za chini za Jasper Cillessen.
Baada ya kona ya David Villa kutokuzaa matunda kwa Hispania, mpira ulisukumwa katikati ya dimba, ikawekwa pasi moja kushoto mwa uwanja kwa Daley Blind. Wakati huo Van Persie yupo katikati ya Jordi Alba na Sergio Ramos.

Van Persie akaagiza krosi iletwe ndani ya box. Kwa kuwa Gerad Pique alikuwa amemshika Arjen Roben, alimuweka Van Persie ‘onside’. Wakati huo Ramos alifanya kosa la jinai kumuacha Van Persie nyuma yake. Casillas akatoka kuja kumlaki, Van Persie alitoka na kichwa kimoja bora sana kwenda nyuma ya wavu wa Iker Casilas.
Namna alivopunguza kasi ili aukute mpira, namna alivopaa na namna alivoupima urefu wa golkipa na goli. Ni kama unaangalia uongo wa superman, spiderman na batman kwa pamoja. That goal was more than sensational.


David Pere
Hilo lilikuwa goli Bora la mashindano kwa upande wangu mimi
Mwajuma
Da hili goli lilishangaza wengi
Samiah
Goli hilo lilinishangaza sana
Aziza mushi
Hilo goli lilikuwa la kipekee na la kihistoria.
Leonard
Van mchezaji mzuri
lombo
dah naikumbuka sana ile siku n ya kihistoria kwa kwel
Emmy cleopa
Ahsante kwa taarifa
Elika
Roben alikuwa mwamba akiwa uwanjani alikuwa hana mpinzani
Theonestina
Lilikuwa Gori la mwaka
warda
VanPersie Amepotelea wapi jamani #Meridianbettz
felister
lile bao hadi madaktari walisahau kuwasikiliza wagonjwa wao
Khadija
Ilikuwa hatari sana mm mwenyewe nilishangaa sana#meridianbettz
Magdalena
Ilikuwa goli la kihistoria
Devotha
Iilikua ni goli la ajabu san
Njiku
Van alikuwa mchezaji bora na mwenye nidhamu akiwa uwanjan namkubal sanaa na goli zuri
Frank Patrick
Kwenye lile kombe la Dunia hili goal la VAN PERSIE ndio lilikuwa Goal bora la mashimdano kwasababu lilikuwa lakipekee sana nikashangaa eti akapewa mtoto James na bao la kawaida sana
Antony Luseno
Mtu aliyekuwa na uwezo wa kufunga unpredictable goals,van persie
Hidaya
Goli la maajabu kwa kweli
Johnmary joel
Huyo mchezaji ni hatari#meridianbetz
Ernest
Hii diving header ya Van Persie utasema kapiga na mguu!!!
Hamidu
Nakumbuka goli Hilo la van persie
Likuwa goli Bora la mashindano.. Enzi zake huyu jamaa alikuwa noma Sana#meridianbettz
Hope mwaikuka
Aisee nlkua cjui hii
Gabriel
Arsenal walipoteza bahat kumuacha van persie aondoke
Sadick
Hapo ndio wapenzi wa mpira tunasuuzika na roho. Hakuna maumivu ya kiingilio bali raha moyoni. Van persie alijitoa mzimamzima#meridianbettz
Theckla
Lilikuwa bonge la goli
Furahav
Huyu jamaa hatari,mana alipaa kama kunguru kufunga goli.
Shafii
Hili goli unbelievable kwa jins lilivyo fungwa van persie alikua straker wa aina yake
Povel
Van persie top striker kwngu mm yupo vzr nakumbuk mbal sana goli lake thnks meridian kwa update
isha
Alitisha sana
Lydia Emmanuel Magoti
Van persie atarii kwasababu aliwashangaza watu kwakombola alilolitoa mtuatarii Sana huyo
Amani
lilikuwa goli Bora la mashindano# meridianbettz
Salma
Fundi huyo
Agness
Duuh jamaa ni noma alishangaza kwa kweli
Neema juma
Van ni mchezajiii mahirii sana kaacha historia
Mwanaidi
Lilikuwa bonge moja la goli aisee
Genia Sikaluzwe
Huyo jamaa ni fundi wa mpira
Dorophina
Tnx meridian makala nzuri nilikuwa sifahamu chochote
Rehema
Huyo jamaa ni fundi
Ester jackson
Hilo goli lilikuwa hatari hakuna shabiki aliye kaa chini
farida ahmadi
Van perse ni mchezaji bora na mzuri Sana hongera Sana kwa goli zuri kama hilo