Kocha wa zamani wa klabu ya Al Ahly na mchezaji wa kimataifa wa Ujerumani mashariki Hans-Jürgen “Dixie” Dörner amefariki dunia alikiwa na miaka 70 baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Dörner ambaye maisha yake yote ameichezea klabu ya Dynamo Dresden ambayo alishinda nayo makombe matano ya Ujerumani mashariki na makombe matano, pia amefanikiwa kuichezea timu ya taifa ujerumani masharikimichezo 100 na alikuwepo kwenye timu iliyoshinda medali ya Olympic mwaka 1976.
Baada ya kustaafu mwaka 1985 Dörner akijikita kwenye tasnia ya Ukocha na alianza kufundisha timu ya vijana ya ujerumani mashariki chini ya miaka 23 kabla ya kujiunga na Werder Bremen, FSV Zwickau na Al Ahly mwaka 2000-2001.
Akiwa jijini Cairo kwenye timu ya Al Ahly alifanikiwa kuchukua kombe la Misri Egypt Cup kwa kuifunga Ghazl El-Mahalla, kabla ya kuondoka na kumuachia mikoba mreno Manuel Jose, na baadae akaamua kukaa mbali na maswala ya mpira.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.
CHEZA HAPA